![]() |
| Naibu wa chansela Prof Erastus Njoka amkabidhi Francis makucha |
Tuesday, November 20, 2018
Chuo cha Chuka chawafanyia Fadhila walemavu
Wanasema waswahili kwamba Dau la mnyonge haliendi joshi, na likienda litazama. Naibu wa chansela hakukubali kuliona dau la mwanafuni Francis Wanyama likizama. Ndipo akaamua kumfanyia francis fadhila kwa kumtunuku makucha mapya {crutches} kwani aliyokuwa akiyatumia yalikuwa yamechakaa. Kuterema kwa wanyama hakungefichika kwani alivaa tabasamu isiyo elezeka alipokuwa akikabidhiwa makucha yale. Chuo kikuu cha chuka kimelivalia njuga swala la kuwajali na kuwakubali wanafunzi na wafanyikazi walio na ulemavu. Chuo cha Chuka kimehakikisha kwamba wanafunzi hawa wanatamba na kutambaa katika majengo yake yote. Pamoja na hili, kitengo cha ushauri nasaha kimehakikisha kwamba unyanyapaa haupo miongoni ma wanafunzi wengine kwa kuwahamasisha umuhimu wa kuwakubali na kuwapenda wenzao waliolemaa. Aidha, prof. Erastus Njoka alitoa wito kwa jamii kuwapa elimu ya kutosha walemavu kwani wanauwezo na maarifa kama watu wengine wasio na ulemavu.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)

No comments:
Post a Comment