Tuesday, November 20, 2018

Chuo Cha Chuka chainuka





 Chuo Cha Chuka cha wavutia walio na tamaa ya kupata elimu

Chuo kikuu cha Chuka Kinaendelea kuinuka kwa kasi ya kuduwaza. Chuo hiki ni mojawapo ya vyuo ambavyo vilianzishwa chini ya miaka kimi na tano {15] iiyopita. Hata hivyo, kuongezeka ka idadi ya wanafunzi kadri miaka inavyo songa kutoka wanafunzi mia tano{500} chuo kilipoanza , hadi wanafunzi elfu kumi na saba {17000} sasa hivi ni dhihirisho tosha kwamba Chuo hiki kinaingia katika orodha ya vyuo vya kimataifa. Aidha, usimamizi wa Chuo cha Chuka ukiongozwa na Naibu wa Chansela Prof Erastus Nyaga Njoka unajizatiti kujenga mijengo ya kisasa ambayo itaendana na hadhi na viwango vya juu vya elimu chuoni humo. Miongoni mwa majengo hayo ni pamoja na Bweni la wanafunzi wa kiume, kituo cha utafiti cha kisasa na umbo au jengo tawala ambalo linatazamiwa kuwa kivutio kikubwa na uti wa mgongo wa chuo hicho. Bila shaka ni Dhahiri kwamba Chuo Cha Chuka kinaenziwa na wengi na kitaendelea kuwavutia wengi walio na ari ya kukifu kiu ya elimu na maarifa.
Bweni la wanafunzi wa kiume 


Umbo Tawala litakalo kuwa kivutio kikuu chuoni Chuka{administration block}

No comments:

Post a Comment