Chuo Cha Chuka cha wavutia walio na tamaa ya kupata elimu
Chuo kikuu cha Chuka Kinaendelea kuinuka kwa kasi ya
kuduwaza. Chuo hiki ni mojawapo ya vyuo ambavyo vilianzishwa chini ya miaka
kimi na tano {15] iiyopita. Hata hivyo, kuongezeka ka idadi ya wanafunzi kadri
miaka inavyo songa kutoka wanafunzi mia tano{500} chuo kilipoanza , hadi
wanafunzi elfu kumi na saba {17000} sasa hivi ni dhihirisho tosha kwamba Chuo
hiki kinaingia katika orodha ya vyuo vya kimataifa. Aidha, usimamizi wa Chuo
cha Chuka ukiongozwa na Naibu wa Chansela Prof Erastus Nyaga Njoka unajizatiti
kujenga mijengo ya kisasa ambayo itaendana na hadhi na viwango vya juu vya
elimu chuoni humo. Miongoni mwa majengo hayo ni pamoja na Bweni la wanafunzi wa
kiume, kituo cha utafiti cha kisasa na umbo au jengo tawala ambalo linatazamiwa kuwa
kivutio kikubwa na uti wa mgongo wa chuo hicho. Bila shaka ni Dhahiri kwamba
Chuo Cha Chuka kinaenziwa na wengi na kitaendelea kuwavutia wengi walio na ari
ya kukifu kiu ya elimu na maarifa.
 |
| Bweni la wanafunzi wa kiume |
 |
| Umbo Tawala litakalo kuwa kivutio kikuu chuoni Chuka{administration block} |
No comments:
Post a Comment