Wanafunzi wa chuo cha Chuka Wachagua Viongozi
o
Baada ya muda wa kampeni na ahadi kochokocho kama ilivyo ada ya wanasiasa, siku ya kuwapima mizana wawaniaji wa nafasi tofauti iliwadia. Kwa kuwa chuo hiki kina vitivo 5 wawakilishi 15 wa wanafunzi hususan watatu kutoka kila kitivo mnamo januari 26 mwaka huu walijitosa katika uga wa pavilion kuwachagua viongozi.
Kwa kuwa chuo kikuu cha chuka kina enzi demokrasia, wanafunzi walipata fursa ya kuwania nafasi tofauti za uongozi katika chama cha wanafunzi .{Chuka University Students A ssociation}.
Uchaguzi wa mwaka huu ulikuwa tofauti kwani bunge la kitaifa lilibatilisha mfumo wa awali ambapo wanafunzi waliruhusiwa kuwachagua viongozi moja kwa moja, hadi mfumo wa wawakilishi wa vitivo tofauti kuwachagua viongozi kwa niaba ya wanafunzi.
Shughuli nzima ya uchaguzi iliendelea bila bighudha yoyoyte ikizingatiwa kwamba chuo kilikuwa kimewaalika maafisa wa tume ya uchaguzi nchini ili kuendesha mpango huu pamoja na vitengo vya usalama vilivyokuwa vimeshika doria
Baadhi ya walio ibuka washindi ni pamoja na Livan Njeru, mwenye kiti,james kamau, katibu mkuu, paul ogeto, mweka hazina, moureen nyambura, katibu mwandaliza, john Momanyi, mwelekezi wa masomo na Josphat Maru, mwelekezi wa ustawi wa wanafunzi. Viongozi hawa walichukua rasmi jukumu la kilisukuma gurudumu la kuhakikisha ustawi wa wanafunzi umeshughulikiwa kwa kina.
“Hatuku kumbana na changamoto zozote za utovu wa nidhamu kama ilivyo kawaida ya chaguzi za vyuo vingine zinazo kumbwa na fujo na uharibifu wa mali.” Daktari Geodfrey Gathongo ambaye ni mwenye kiti wa tume ya uchaguzi alidokeza. Akishadidida haya, Joyce Macharia ambaye ni naibu wa mwamini wa ustawi aliwapongeza wanafunzi wote kwa nidhamu na utulivu unaoendelea kukipa chuo cha Chuka haiba na turuhani zisizo na kifani.
Katibu Mkuu
Mwenye Kiti
Kikundi cha wasakata densi cha New Blyden cha Chuka kilipata nafasi ya kuonyesha umahiri wao katika densi kwenywe kipindi maarufu sana nchini kenya{Churchil Show Meru Edition} baada ya kuibuka washindi kati ya vikundi ishirini. Kikundi hiki kilizinduliwa mwaka wa 2015 ambapo kilikuwa na wanachama watanonpeke yake. Kusudio la waanzilishi lilikuwa kuimarisha talanta sio tu katika densi bali pia sarakasi, michezo ya kuigiza na pia vichekesho. Bali na hayo New Blyden wamebobea kwa Sanaa licha ya changamoto nyingi kama vile kukosa ufadhili wa kifedha ili kuendeleza shughuli zao za kuimarisha talanta katika densi. Sasa hivi, New Blyden ni nyumbani kwa burudani kwa takriban wanafunzi nia moja ambao husakata densi katika warsha mbalimbali chuoni Chuka na pia sherehe zingine kama vile harusi.” Densi ina manufaa mengi kwani inawawezesha wengi kukifu mahitaji yao na hata kuanzisha biashara kutokana na malipo wanayo yapata baada ya kuburudisha hadhira. Aidha densi pia inamwezesha mwanafunzi kuepukana na tabia kama vile u;languzi wa dawa za kulevya , uasherati na pia kuweka dau almaarufu {Kamari}. “alidoke Nicholus Muriki mwenye kiti wa kikundi hiki. New Blyden wanatoa shukrani za dhati kwake Joyce Macharia ambaye ni naibu mwamini wa wanafunzi kwa juhudi zake kuhakikisha kwamba kikundi hiki kimepata fursa ya kuburudisha katika sherehe za chuo cha Chuka





Amazing work.keep on
ReplyDeleteKazi yako ina mvuto wa kisanii. Hii ni ishara tosha kuwa una kipaji cha uandishi.kila laheri.
ReplyDeleteasante sana. Kwa makadara ya mwenyezi nitaendelea kubobea katika uandishi wangu.
DeleteExcellent piece of art.keep up James
ReplyDeleteInapendeza kaka. Endelea. Unapishaaaa
ReplyDeleteIn love with your work. Keep it up. That Swahili joh😍😍😍
ReplyDelete